Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

ILI KUUNDA CHAMA KIMOJA CHA UPINZANI CHENYE NGUVU, MBATIA ANENA HAYA…

mbatia
Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), James Mbatia, amesema ili kuweza kuanzisha chama kimoja cha upinzani chenye nguvu, inahitajika viongozi wa upinzani kujenga msingi wa uaminifu miongoni mwao.

Pamoja na kwamba hakutaka kutamka wazi kuwa uaminifu huo kwa sasa haupo, Mwenyekiti huyo pia wa Chama cha NCCR-Mageuzi, amesisitiza kuwa bado lengo la kuanzisha chama hicho kimoja cha Ukawa lipo palepale na linaendelea kufanyiwa kazi.

Mbatia alikuwa akihojiwa katika kipindi kinachorushwa kila Jumapili na Televisheni ya Azam. Alisema katika kuanzisha chama hicho, suala la uaminifu miongoni mwa viongozi ni muhimu ili kufikia malengo halisi ya uanzishwaji wa chama hicho.

“Hata mwaka 1964 hayati Baba wa Taifa Julius Nyerere pamoja na Abeid Amaan Karume, waliaminiana kwanza na kwa kutumia utashi wao wakaunganisha nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa Tanzania. Waliamiana,” alisisitiza.

Alipohojiwa kwamba, kwa sasa Ukawa hakuna uaminifu ndio maana bado uanzishwaji wa chama hicho unasuasua, mbunge huyo wa Vunjo, aligoma kueleza kwa uwazi zaidi kusisitiza kuwa uaminifu ni lazima katika suala nyeti kama hilo.

Alisema kwa sasa azma hiyo ya kuwa na chama kimoja imeanza kuonekana zaidi kwa vitendo kuliko maneno kwani kupitia umoja huo walisimamisha mgombea mmoja wa urais hali iliyowapatia mafanikio.
“Ni kweli kwenye umoja wetu kuna migongano ya hapa na pale lakini hiyo ni kawaida lazima tuwe na fikra tofauti, lakini tungefikiria kwenye chanya zaidi ila bado kuna haja ya kujengeana uaminifu kwanza,” alisema.
Aidha, alisema uanzishwaji wa Ukawa ni wazo la NCCR-Mageuzi kwa kuwa tangu chama hicho kilipoanzishwa mwaka 1991 kilikuwa na lengo la kuunganisha nguvu ya upinzani.
“Kwa maana hiyo Ukawa ni mtoto wa NCCR-Mageuzi ambayo ni mama wa upinzani. Kususia vikao vya Bunge Akizungumzia kitendo cha wabunge wa upinzani kuendelea kususia vikao vya Bunge pindi inapotokea kutoelewana ndani ya chombo hicho, Mbatia alisema hiyo ndio njia pekee ya kupatiwa haki wanayoidai badala ya kukaa kimya.”
Hata hivyo, alipobanwa na kuhojiwa kwa nini wasitumie fursa waliyonayo na kubaki ndani ya Bunge na kuwasilisha maoni yao, alisema hiyo ni njia mojawapo ya kuonesha hasira waliyonayo juu ya mfumo uliopo unaoliendesha bunge hilo.
“Hakuna mtu aliyesomea kuwa mbunge au Rais, mabunge yote yaliyopita yaliyoongozwa na Samuel Sitta na Anne Makinda, yote yalikuwa na malalamiko, lakini Bunge hili la 11 malalamiko yamezidi. Ndio maana na sisi tunaamua kutoka ikiwa ni njia ya kuonesha hasira hasa pale tusiposikilizwa,” alisema.
Kuhusu hoja kwamba kwa sasa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, Ukawa imeanza kudhoofu, Mbatia alikanusha hoja hiyo na kusisitiza kuwa kwa sasa umoja huo ndio umeonesha mshikamano hasa kutokana na matukio ya bungeni.

Ukawa na nguvu za Chadema Pamoja na hayo, Mbatia alisema kitendo cha Ukawa kuinufaisha zaidi Chadema kwa kuwapatia wabunge wengi ni jambo lililotegemewa kwani hata mwaka 1995 NCCRMageuzi nayo iliposimamisha mgombea urais aliyekuwa na nguvu kipindi hicho, ilijipatia umaarufu na mafanikio ya kisiasa.

Maridhiano bungeni Aidha, mbunge huyo alipongeza jitihada za Spika wa Bunge, Job Ndugai za kurejesha maridhiano yaliyovunjika katika mkutano uliopita baina ya wabunge wa upinzani na chama tawala na kusisitiza kuwa hatua za spika huyo ni jambo zuri la kuungwa mkono.

Alisema kinachotakiwa ndani ya chombo hicho ni kuhakikisha taratibu zilizowekwa zikiwemo kanuni za Bunge zinafuatwa huku akiendelea kumtupia lawama Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwa ndiye tatizo la mvurugano ndani ya chombo hicho.
“Hata hivyo, Tanzania hii ni yetu sote, keshokutwa tunakutana na viongozi wa dini zote kuzungumza suala la amani ya nchi yetu. Naamini juhudi hizi zikiendelea tutafikia mahala pazuri,” alisema.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top