Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MABOSI MAN U WAMPA MASHARTI MAPYA JOSE MOURINHO KUACHANA NA SERA YA KUNUNUA WACHEZAJI WAZEE

Kocha mwenye makeke mengi Jose Mourinho ameelezwa na mabosi wa Manchester United kubadili mbinu zake za usajili baada ya kuwa na msimu mbaya katika dirisha la  usajili 
Mashetani hao wekundu waliweza kunasa sahihi za wachezaji watatu tu na  Mourinho amekasirishwa kwa Ofisa Mkuu Ed Woodward kushindwa kumuongezea wachezaji wengine.
Linatabainisha Gazeti la The Mirror , Mourinho ameambiwa na mabosi wake pale  Old Trafford kubadilisha sera yake ya usajili kwa kutupia macho zaidi wachezaji wenye umri mdogo na wenye vipaji wanaoweza kudumu zaidi. 
Ripoti zinadai maofisa wa  United wamemuonya  Mourinho kuacha kununua wachezaji wenye umri mkubwa na wenye gharama ambao wanakaribia kustaafu soka  badala yake ajikite katika kuvumbua vipaji 
Mourinho baada ya kuingia Old Trafford  aliweza kumnunua Zlatan Ibrahimovic, Alexis Sanchez na  Nemanja Matic na wengine ambao umri wao ni miaka  28 au zaidi walipokuwa wanajiunga na klabu hiyo kwa kandarasi nono . 
Woodward aliamua msimu huu kutoruhusu kuondoka kwa Paul Pogba na  Anthony Martial, japokuwa  Mourinho alitamani waondoke.
Wafaransa hao ambao ni hazina ya muda mrefu katika klabu hiyo kutokana na kuwa umri mdogo hivyo kuona watawafaa kwa kucheza muda mrefu .
Bodi ya wakurugenzi ya United imeamua kuanzia sasa sera za usajili kuangalia zaidi wachezaji wenye manufaa ya muda mrefu ili kuendana na kasi ya Manchester City, ambao wamenunua wachezaji wenye umri na wenye vipaji na kuwaendeleza kama afanyavyo  Pep Guardiola. 
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top