Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MENEJA ARSENAL ALAUMU USAJILI MBOVU

Arsenal walianza vyema mechi dakika za kwanza tano na pia wakakamilisha kipindi cha kwanza vyema Aubameyang na Henrikh Mkhitaryan wakikaribia kufunga.
Waliwachezea wachezaji wawili wapya, Mgiriki Sokratis Papastathopoulos beki wa kati aliyetokea Borussia Dortmund, na kiungo wa kati kinda wa miaka 19 Guendouzi aliyekuwa akichezea Lorient ya Ufaransa.
Guendouzi alicheza vyema na anataraiwa kuchezeshwa zaidi na Emery Unai msimu huu.
"Ilikuwa mechi yake ya kwanza Ligi ya Premia. Ana sifa nzuri na ustadi pia na akiwa uwanjani ataimarika haraka zaidi," alisema meneja wa Arsenal.
Kulikuwa na dalili kwamba Arsenal ambao walicheza kwa mfumo wa 4-2-3-1 wanahitaji muda zaidi kuzoea mfumo huo mpya.
"Matokeo yalikuwa 2-0 lakini nafikiri kwa jumla katika dakika hizo 90 tulikuwa tunaimarika," Emery alisema.
"Kipindi cha kwanza hatukucheza tulivyotaka. Tulizungumza wakati wa mapumziko kuhusu kuwajibika zaidi kipindi cha pili, kujituma zaidi. Tulitaka tuimarisha udhibiti wa mpira na kuzuia pasi zao. Nafikiri katika kipindi cha pili tulicheza zaidi jinsi tulivyotaka."
Meneja huyo wa zamani wa Sevilla na Paris St-Germain alisema alifurahia mandhari Emirates.
"Tulitaka kuanza hapa na wafuasi wetu. Tulitaka kuonyesha ustadi wetu lakini ni wazi kwamba mikononi mwa Manchester City hatungeweza kuwapa (mashabiki) ushindi. Lakini nafikiri hapa mambo yatakuwa sawa sana."
Arsenal na Unai Emery walikuwa na ratiba ngumu ya mechi kwani sasa wanajiandaa kwa safari ya Stamford Bridge kukutana na Chelsea Jummaosi. City watakuwa wenyeji wa Huddersfield Jumapili.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top