Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

FERGUSON ACHUKIZWA NA ULINZI

Sir Alex Ferguson, meneja wa Manchester United, Jumamosi alielezea kwamba hajawahi kuona ulinzi mbovu wa timu yake msimu huu kama alivoshuhudia wakati timu yake ikiwa ugenini Reading, licha ya kuondoka na ushindi wa magoli 4-3 dhidi ya wenyeji.
 1-0: Reading's Hal Robson-Kanu (centre right) put the home side a goal up after eight minutes
 Robson akifunga goli kwa kicwa kunako dakika ya 8 ya mchezo na kuwafanya reading kuongoza kwa goli 1.Picha na Daily Mail.

United mara nyingi walionekana dhaifu kutokana na mchezo wa kupanga na kuviziana, na meneja Ferguson alisema ni lazima timu yake kuinua kiwango cha mchezo wao kufikia mwishoni mwa wiki ijayo, wakati watakutana na majirani Manchester City.
 1-1: Anderson equalised for Manchester United shortly afterwards
 Anderson akipiga mkwaju ulienda moja kwa moja wavuni likiwa ni goli la kusawazisha kwa Manchester United.Picha na Daily Mail.

"Ulikuwa ni ulinzi mbovu zaidi msimu huu," alielezea Ferguson.
“Lazima tuchukue hatua kuhusu hili”.
 1-2: Wayne Rooney found the bottom corner with a penalty to give United the lead after Jonny Evans had been fouled
 Rooney akitumbukiza kwenye kamba mkwaju wa Penati na kuifanya Manchester United Kuongoza kwa 2 kwa 1 la Reading.Picha na Daily Mail.

"Reading waliweza kuelekeza mipira vyema, lakini kabisa mlikuwa hamna ushindani katika kuzuia hayo."
 2-2: Adam Le Fondre (centre) scores a header to restore parity once again
Adam Le Fondre katikati akiisawazishia Reading kwa kufunga goli la pili,hivyo mchezo kurudi tena kuwa mgumu kwa pande zote mbili.Picha na Daily Mail.

Mara mbili walilemewa na kuwaacha Reading kutangulia kwa magoli, na hii ikiwa ni mara ya 14 msimu huu kuiacha timu ya upinzani kutangulia kupata bao la kwanza.


Magoli yote saba ya timu zote mbili yalifungwa katika dakika 34 za kipindi cha kwanza katika uwanja huo wa Madejski.
 3-2: Reading then took the lead with another header through Sean Morrison
 Reading walichukua usukani kwa muda pale Morrison alipoifungia timu hiyo goli la 3 kwa 2 ya Manchester United na kuwaweka katika wakti mgumu Man U.Picha na Daily Mail.
3-3: Wayne Rooney levelled things again with a close-range finish from Patrice Evra's cut back
Rooney akitumia pasi murua toka kwa Evra akiirudisha mchezoni timu yake kwa kuisawazishia goli la 3 hivyo ngoma kuwa Reading 3 na 3 Manchester United.Picha na Daily MAil.

Kwa bahati nzuri, Man U waliweza kujibu mashambulizi ya Reading mara mbili, na kuongezea magoli ambayo yaliwawezesha kurudi Old Trafford na ushindi, na wakiwa kileleni mwa ligi ya Premier, sasa tofauti kati yao na wapinzani wao wakuu, majirani Man City, ni pointi tatu.
 3-4: Ten minutes before half-time, Robin Van Persie raced through to score what proved to be the winner
Van Persie akaifungia timu yake shuti lililoamua mshindi wa mechi hiyo kwa kuifungia Manchester UNited goli la 4 hivyo kuondoka na pointi tatu muhimu.Picha na Daily Mail.

Man City, wakiwa nyumbani katika uwanja wao wa Etihad, watawakaribisha Man United Jumapili ijayo.

"Tulistahili kutandikwa leo," alisema Ferguson. 


"Hakuna aliyefanya juhudi za kushindania migongeo. Pasipo kupendelea, Reading walimiliki mpira vyema, kijana [Nicky] Shorey aliwaelekezea wenzake mipira vyema mno. Tulistahili kufanya vyema zaidi ya hivyo. Tulicheza vibaya mno”, alilalama Ferguson.


"Iwapo utafanya makosa kama hayo katika ulinzi, basi kila wiki kazi yako itakuwa ni juhudi za kuokoa tu. Leo ilikuwa ni juhudi zaidi za kuokoa tu.
"Ilikuwa ni muujiza namna tulivyoshinda kwa ulinzi kama huo. Ninaridhika tu kwa kuwa tuliondoka na ushindi.” 

Chanzo cha Habari;www.bbc.co.uk/swahili
Picha na daily Mail
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top