Natoa Jambo sana kwenu nyote:
Nilipata
maswali kwa watu ambao walionyesha nia ya kutaka kuambatana na mimi na
crew yangu kwenda kuukwea Mlima mrefu Afrika, Kilimanjaro.
Na mimi bila hiana nimeona si vibaya nikiwafahamisha utaratibu wote, ili kwa atakaeweza kushiriki tuongozane nae pamoja
Tutaondoka Dar es salaam kuelekea Moshi tar 6 January 2013
Kwa njia ya anga...
Kwa
wanaotokea Dar au mikoa mingine watalazimika kujilipia nauli za Ndege au
Bus au kama ni magari yao binafsi ni sawa pia, ila tar 6 January 2013
tunakutania Moshi, Kilimanjaro.
Tutalala hapo kwa usiku mmoja huku tukisubiri kuianza safari ya Mlimani siku inayofuata.
Gharama za safari ya kupanda mpk kileleni na kushuka ni US$ 500 (Dola za kimarekani mia tano) kwa mtu mmoja
Hiyo
gharama ina cover Milo mitatu kwa siku, Wabeba mizigo, Guides, Chef,
Camping gears na Hifadhi ya kulala tangia siku unapofika Moshi mpk siku
utakayoondoka
Japo kuna vitu kadhaa utalazimika kununua kwa gharama tofauti na hiyo endapo utavihitaji.
Vitu kama Pombe, mavazi ya baridi ya kuongezea n.k
Tunaanza
kupanda Mlima tar 7 January 2013 na tar 12 January 2013 tunakuwa
tumekamilisha safari yetu hiyo, itakayotuchukua siku 5.
Kuhusu maswala ya afya kila mtu anafahamu afya yake ni muhimu mkajiangalie kwa madaktari mpate ushauri kabla ya kuamua kwenda kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mimi binafsi niko fiti, ki afya na kimazoezi.
La msingi zaidi linaloshauriwa ni kutayarisha fikra zako tu ziwaze kupanda na kumaliza bila pupa,
Ukianza uoga tu hufiki juu.
Oooh watu wanaugua, watu wanakufa wewe jiamini bwana.
Waliopanda wakafika wana nini mpaka si tushindwe?
Gate tutakaloondokea ni MARANGU GATE
Natumaini kwa maelezo hayo mtakuwa mmepata kufahamu vya kutosha na kuamua kama mnakuja na mimi au la??
Ukiwa tayari kwenda tuwasiliane ili ni comfirm idadi ya watu.
Deadline ni tar 1 January 2013.
Niandikie e-mail: judyjaydee@yahoo.com
Subject iwe: MT.KILIMANJARO ili nipate urahisi wa kuzifungua mail zinazohusiana na safari hiyo
Niwatakie heri ya mwaka mpya in advance.
Kuhusu maswala ya afya kila mtu anafahamu afya yake ni muhimu mkajiangalie kwa madaktari mpate ushauri kabla ya kuamua kwenda kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mimi binafsi niko fiti, ki afya na kimazoezi.
La msingi zaidi linaloshauriwa ni kutayarisha fikra zako tu ziwaze kupanda na kumaliza bila pupa,
Ukianza uoga tu hufiki juu.
Oooh watu wanaugua, watu wanakufa wewe jiamini bwana.
Waliopanda wakafika wana nini mpaka si tushindwe?
Gate tutakaloondokea ni MARANGU GATE
Natumaini kwa maelezo hayo mtakuwa mmepata kufahamu vya kutosha na kuamua kama mnakuja na mimi au la??
Ukiwa tayari kwenda tuwasiliane ili ni comfirm idadi ya watu.
Deadline ni tar 1 January 2013.
Niandikie e-mail: judyjaydee@yahoo.com
Subject iwe: MT.KILIMANJARO ili nipate urahisi wa kuzifungua mail zinazohusiana na safari hiyo
Niwatakie heri ya mwaka mpya in advance.
Much Love to you all:
JIDE
JIDE
Chanzo: http://ladyjaydee.blogspot.com
Post a Comment