Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AKABIDHI BAJAJ MPYA KWA MLEMAVU WA MIGUU,MJINI DODOMA

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi bajaji mpya mlemavu wa miguu ambaye ni mfanyakazi wa TANROADS Bi.Sarah Nalingigwa Nkumbo huko ikulu mjini Dodoma leo asubuhi. Kulia ni Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli.Wapili kushoto ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete na kushoto ni mkurugenzi Mkuu wa TANROADS Injinia Patrick Mfugale. Bi. Sarah ambaye ni Mfanyakazi wa TANROADS mkoani Singida alikabidhiwa Bajaji hiyo ikiwa ni ahadi ya Rais alipokuwa akifungua Barabara ya Manyoni- Itigi.
Picha na Freddy Maro-IKULU
----
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Februari 10, 2013 amekabidhi pikipiki aina ya bajaj kwa mama mmoja mlemavu, Mama Sarah Mkumbo Nalingigwa katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu Ndogo mjini Dodoma.

Mama Nalingigwa ni mtumishi wa Wakala wa Barabara nchini – TANROADS- katika Mkoa wa Singida na shughuli ya leo imehudhuriwa pia na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Patrick Mufugale na Mama Salma Kikwete.

Shughuli ya makabidhiano ya leo, inatimiza ahadi ambayo Mheshimiwa Rais aliitoa kwa Mama Nalingigwa wakati alipokutana naye miongoni mwa wananchi waliohudhuria sherehe ya utiaji jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mjini Itigi, Mkoa wa Singida Novemba mwaka jana.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hiyo, Rais Kikwete amemwambia mama huyo: “Nimefurahi kwamba nimeweza kutimiza ahadi yangu. Hii ndiyo faraja yangu kwamba sasa utaweza kufanya kazi zako kwa urahisi zaidi, utaweza kutembea kwa urahisi zaidi na kufika kazini na kurejea nyumbani kwa namna ya haraka zaidi.”

Naye Mama Nalingigwa amemwambia Rais Kikwete: “Wewe ni kiongozi shupavu, kiongozi hodari na mpiganaji anayemjali kila mtu. Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akujalia ili uendelee kuwaona wengine wenye mahitaji kama ya kwangu.”

Ameongeza mama huyo ambaye amefanya kazi Wizara ya Ujenzi kwa miaka 30 iliyopita: “Kwa kuniwezesha kiasi hiki, umenipa uwezo wa kufanya kazi kwa namna bora zaidi., Ni vyema kuwa viongozi wengine wakaiga mfano wako wa kujali watu walioko chini yako.”
Amesisitiza: “ Sisi walemavu tuna mahitaji mengi na hivyo naomba unedelea kutuangalia kwa jicho la huruma na kutupunguzia vikwazo vya maisha kila nafasi inapojitokeza.”
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top