Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

WABUNGE 47 WAJIUNGA MAFUNZO JKT

JUMLA ya wabunge 47 kutoka vyama CCM, Chadema na NCCR-Mageuzi, wamekubali kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa ajili ya mafunzo na uzalendo kwa taifa.
Habari za kuaminika zilizopatikana mjini Dar es Salaam jana na kuthibitishwa na Makao Makuu ya JKT, zinasema wabunge hao wametawanywa katika vikosi mbalimbali na wanatakiwa kuripoti kwenye vikosi vyao kunzia Machi mosi, mwaka huu.

Msemaji wa JKT, Meja Emmanuel Mruga, alipoulizwa kuhusu wabunge hao kujiunga na jeshi hilo, alisema mpaka sasa wana orodha ya wabunge 47 kutoka vyama mbalimbali.

Alisema wabunge hao, wametawanywa katika kambi mbalimbali kwa ajili ya mafunzo ambayo yatarajia kuanza mwezi ujao.

Alisema wabunge hao, waliomba wenyewe kwa ajili ya kupata mafunzo ambayo wanaamini yatawajengea uzalendo zaidi kwa taifa lao.

Baadhi ya wabunge ambao MTANZANIA imepata majina yao na vyama wanavyotoka kwenye mabano ni David Kafulila (NCCR-Mageuzi), Zitto Kabwe (CHADEMA), Halima Mdee (CHADEMA), Freeman Mbowe (CHADEMA), Abdulkarim Shaha (CCM), Esther Bulaya (CCM), Twaida Galusi (CCM), Neema Hemed (CCM), Ezekiel Wenje (CHADEMA), Joshua Nassari (CHADEMA), Raya Ibrahim (CHADEMA), Godbless Lema (CHADEMA) na Nyambari Nyangwine (CCM).

Akizungumzia mafunzo hayo, Zitto Kabwe alisema kuanzia sasa anajiandaa kuanza maisha mapya ya jeshi na atapumzika siasa kwa muda wa miezi sita.

“Najiandaa kupumzika siasa, kwa ajili ya kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), nadhani ni hatua nzuri ambayo tunataka kuwaonyesha Watanzania wazalendo na vijana wenzetu,” alisema Zitto.

Naye Mdee, alisema zaidi ya robo tatu ya wabunge wote vijana wa chama hicho, waliomba kujiunga JKT na tayari wamepangwa katika vikosi mbalimbali.

“Si mimi na Zitto, nakwambia karibu robo tatu ya wabunge vijana wa CHADEMA, tumeamua kujiunga kwenye mafunzo ya JKT,” alisema Mdee.

Alisema yeye amepangwa kikosi cha 842 KJ kilichopo Mlale, mkoani Ruvuma.

Alisema wengine ni Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, ambaye amepangiwa kikosi cha JKT Ruvu, Mkoa wa Pwani.

Habari zinasema Mbowe aliomba kujiunga JTK na amepangiwa kambi moja mkoani Tabora.

Akizungumzia sababu za kujiunga na jeshi hilo, Mdee alisema wanataka kujifunza mambo tofauti yatakayowasaidia kutekeleza wajibu wao wa kisiasa na kijamii sawasawa.

“Unajua sisi ni viongozi wa watu, tunadhani mafunzo ya kijeshi yatatusaidia kutekeleza kazi za kila siku, kujifunza ukakamavu, na zaidi kwa vipi tunaweza kujilinda kwa mantiki ya usalama binafsi.

“Kingine ni kujifunza kazi za kila siku za maisha, kiuchumi, kijamii, kilimo na vitu kama hivyo ukizingatia sisi ni viongozi tunaopaswa kuongoza watu, hususani wapiga kura kwa mifano.

Kuhusu kujifunza zaidi uzalendo kama ambavyo imekuwa ikisemwa na viongozi serikalini, Mdee alisema uzalendo ni tabia ya mtu binafsi na kamwe jeshi haliwezi kumfundisha mtu uzalendo.

“Ninakubaliana na suala la nidhamu, jeshi linaweza kumfundisha mtu nidhamu, lakini siyo uzalendo.

“Walioharibu nchi na kuitumbukiza katika ufukara na ufisadi karibu wote wamepitia jeshini, hatuna cha kujifunza kwao kutokana na kwenda kwao jeshini,” alisema na kuongeza:

“Ngoja twende huko tukajifunze mambo ya ziada, naamini tutapata kitu cha ziada kwa ajili yetu na jamii tunayoiongoza”.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top