MWANDISHI
wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa upande wa Televisheni
Florence Dyauli amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya
Rabininsia memorial iliyopo jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa kutokana kusumbuliwa
na maradhi ya Nimonia
Taarifa iliyotolewa jana na
ofisi za TBC ilisema kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Nimonia
na alilazwa kwa ajili ya matibabu hadi jana usiku mauti ilipomfika.
Taratibu za mazishi
zilikuwa bado hazijafanyika na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali
hiyo ya Rabininsia ukisubiria taratibu za mazishi kutoka kwa ndugu wa familia.
Florence alizaliwa Julai
27, 1961 ambapo alipata elimu yake ya msingi kuanzia 1968 hadi mwaka 1975
katika shule ya Msingi Chang’ombe iliyopo jijini Dar es salaam.
Alifanikiwa kujiunga na
elimu ya Sekondari katika shule ya Kisutu girls kati ya mwaka 1976 hadi 1979.
Baadae alijiunga na chuo cha Tabora secretarial College kuanzia mwaka 1980 hadi
1981 na kujipatia mafunzo ya cheti cha ukarani.
Mnamo mwaka 1986 hadi 1988
alijiunga na chuo cha uandishi wa habari kwa ngazi ya stashahada ya uandishi wa
habari.
Aliniajiriwa kama mwandishi
wa habari msaidizi katika kituo cha Radio Tanzania Dar es salaam kuanzia 1982
hadi Novemba 1999.
Kisha mwaka 1994 hadi
Novemba 1999 alikuwa Shift Editor .
Hadi mauti inamkuta,
marehemu alikuwa mwandishi wa habari daraja la kwanza kwa upande wa Televisheni
ya Taifa TBC.
Post a Comment