Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MKE WANGU ANA MIMBA YA MWANAUME MWINGINE, JE SHERIA INASEMAJE ?.



Image result for mwanamke mwenye mimba
NA  BASHIR  YAKUB -

Wakati  nilipoandika kuhusu  talaka  na  mambo  yanayokubalika  kisheria  kama  sababu  za  talaka  nilipata   maoni  na  maswali  mengi kutoka kwa  wasomaji wetu.  Kati  ya  hao  ni mmoja  ambaye  alijitambulisha  kwa  jina   na  kuwa  ni  mkazi  wa  kinondoni  Dar es  salaam. Huyu  aliuliza  swali  lake  ambalo  ndilo  kichwa  cha  makala  haya.  Alisema  ameziona  sababu  nilizoeleza  ambazo  zinapelekea   mtu  kupewa  talaka  lakini  sababu  inayohusu  tatizo  lake  hakuiona  na  hivyo  aliomba  nimpatie   ufafanuzi. Maelezo  yake  kwa  ufupi  yalikuwa  hivi:

1.KUPATA  MIMBA  NJE  YA  NDOA.

Ndugu  huyu  alichoeleza  ni  kuwa  yeye ni  muajiriwa  katika jeshi  la  Wananchi  wa  Tanzania.  Na  kuwa  mwaka  jana   alipangiwa  safari  ya kikazi   kwenda  Congo  kwa  ajili  misheni  maalum  ya  jeshi  kwa  kipindi  cha  miezi  sita.  Anasema  alikwenda  na kumuacha  mke  wake  nyumbani  kwake  ambapo  amerudi   mwaka  huu . Anasema   ndani  ya  wiki  moja  tangu  arudi  hakuielewa  hali  ya  mke  wake kitu  kilichomfanya  achukue  maamuzi  ya  kumpeleka  hospitalini  kwa  ajili  ya  vipimo.  Alifanyiwa  vipimo  vyote  na  hatimaye  kugundulika  ana  mimba  ya  mwezi mmoja.  Swali  la  ndugu  huyu  lilikuwa  ni  sheria  inasemaje  katika  hali  kama  hiyo.

2.  SHERIA  INAVYOSEMA  KUHUSU  HILI.

Ndani  ya sura  ya  29  ya  sheria  ya  ndoa  kuna  mambo  makuu  matatu. Kwanza  kuna  kitu  kinaitwa ndoa  halali ( valid  marriage ),  pili  kuna  kitu  kinaitwa  ndoa  haramu ( void  marriage)  na  tatu  kuna  kitu  kinaitwa ndoa  halali  au  haramu  kutegemea  na  uamuzi  wa moja  wa  wanandoa ( voidable  marriage).
Katika  hayo  matatu  ,mawili  ya  ndoa  kuwa  halali  na  ndoa  kuwa  haramu  yanajulikana  vyema   ambapo  halali  ni  halali,  ni  ile  ambayo  haina  shida  na  haramu   ni  haramu,  ni  ile  ambayo  hairuhusiwi.  Pengine  maelezo  yanaweza  kutakiwa  katika  hili  la  tatu  la  ndoa  kuwa  halali  au  haramu  kutegemea  maamuzi  ya  mmoja  wa  wanandoa( voidable  marriage ).

3. UHALALI  AU  UHARAMU  WA  NDOA  KUTEGEMEA  NA  UAMUZI  WA  MWANANDOA.

Kifungu  cha  39  cha  sheria  ya  ndoa  kimeeleza  mambo  manne    ambayo  yakitokea  katika  ndoa  uamuzi  wa  ndoa  hiyo  kuendelea  au  kutoendelea  utakuwa  katika  mikono  ya  mmoja  wa  wanandoa  hao. Hii  ina  maana  mmoja  akiamua  ndoa  iendelee  hata  kama  limetokea  jambo  hilo  itaendelea halikadhalika  akiamua  isiendelee  basi   taratibu  za  kuachana  zitafanyika.  Mambo  hayo  ni  kama  yafuatayo :

( a ) Ikiwa  mwanaume  au  mwanamke  ataishiwa  na  uwezo  wa  kujamiiana. Mara  nyingi  tatizo  hili  hutokea  kwa  wanaume  ambapo  kutokana  na  ugonjwa  au  sababu  nyingine  yoyote   anashindwa  kabisa  kutekeleza  tendo  la  ndoa tena  kwa  muda  mrefu. Hii  inaweza  kuwa  wakati  wa kufunga ndoa  au   baadae  katika  ndoa.  Hili  likijitokeza  basi  mwanamke  atakuwa  na  hiyari  kutokana  na  mazingira  aliyoyaona  aendelee  kukaa  katika  ndoa  au  amtaliki  mwenzake.  Ni  uamuzi  wake.

( b ) Pili  ni  iwapo  mmoja  kati  ya  wanandoa  amepatwa  na  magonjwa ya  akili  ya  kuchanganyikiwa  na  pengine  ni  tatizo  ambalo  sio  rahisi  kutibika. Mwanandoa  ataamua  kati  ya  kuendelea  na  ndoa  hiyo  au kuachana  nayo.

( c ) Tatu  ni  iwapo  mmoja  wa  wanandoa   amepatwa  na  tatizo  la  magonjwa  ya  kuambukiza  kupitia  kujamiiana(venereal disease). Kwa  mfano  yawezekana  mmoja  akakutwa  na  virusi  vya  ukimwi  na  mwingine  hana japo  wote  walikuwa  katika  ndoa. Ni hiari  ya mmoja  ambaye  hana  au  mwenye  navyo  kuamua  kumtaliki mwenzake au  kuendelea  na  ndoa.

( d ) Nne,  ndio  hili  sasa  ambalo  ndio  mada  yetu. Ikiwa  mwanamke  atagunduliwa  kuwa  na  mimba  ya  mwanaume  mwingine   mbali  na  yule  aliye  naye  katika  ndoa  basi  ni  hiari  ya  mwanaume  huyo  kuamua  kuendelea  na  ndoa  hiyo au  kuachana  nayo. Hivyo  jibu  kwa ndugu  yangu  ni  kuwa  ni  uamuzi  wake  sasa   kuachana  na  ndoa  hiyo au  kuendelea nayo,  vyovyote  itavyompendeza.

Hata  hivyo  katika  kuachana  na  ndoa   katika  mazingira  yote  niliyoeleza  hapa juu taratibu  za  talaka  za  kisheria  ikiwemo  kuihusisha  mahakama  zitahusika.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top