Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Wizara ya Mambo ya Nje yashiriki kusafisha Soko la Temeke kuadhimisha miaka 70 ya UN

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema akitoa hotuba yake kwenye maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa nchini yaliyoambatana na usafishaji wa soko la Temeke Sterio lililopo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho hayo yaliyoanzia mkoani Kilimanjaro kwa kupanda miti ipatayo elfu mbili (2000). Katika Hotuba yake Mhe. Mjema aliwaasa wafanyabiashara katika soko hilo kutunza mazingira ili kudhibiti na kuzuia magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu. Katika maadhimisho hayo Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto) alikabidhi vifaa vya kufanyia usafi kwa Mhe. Mjema  kwa ajili ya kufanyia usafi katika soko hilo ikiwa ni moja ya kuchochea utunzaji wa mazingira katika maeneo ya biashara 
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza kwenye maadhimisho hayo
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez naye akizungumza katika maadhimisho hayo
Juu na Chini: Sehemu ya Watumishi wa Serikali na Umoja wa Mataifa wakisikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika maadhimisho hayo. 
Sehemu ya wadau walioudhuria usafishaji katika soko hilo wakiwa tayari kwa kuanza zoezi la usafi katika soko hilo.
wananchi waliojitokeza wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea 
Mkuu wa Wilaya ya Temeke akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez, akishuhudiwa na Balozi Mushy (kulia) 
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho hayo wakishuhudia Mkuu wa Wilaya yao Mhe. Mjema (hayupo pichani) akikabidhiwa vifaa hivyo. 
Mhe. Sofia Mjema, Bw. Alvaro ( kushoto) na Balozi Mushy (wa pili kulia) wakishiriki kusafisha soko la Temeke Sterio.
Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakishiriki katika zoezi la usafishaji wa soko la Temeke Sterio.
Balozi Celestine Mushy (kulia) akizungumza na vijana wanaofanya biashara katika Soko hilo juu ya umuhimu wa kufanya usafi katika mazingira yanayowazunguka.  
Usafi ukiendelea
Balozi Mushy akizungumza na Waandishi wa Habari waliohudhuria katika maadhimisho hayo.


Picha na Reginald Philip
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top