Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

NYUMBA TISA ZACHOMWA MOTO Z'BAR DK.MAGUFULI AKITANGAZWA MSHINDI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec)
NA RAHMA SULEIMAN

Nyumba tisa zimeteketezwa kwa moto katika kisiwa cha Tumbatu Kaskazini Unguja muda mfupi baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kutangaza ushindi wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli.

Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, baadhi ya wafuasi na wanachama wa CCM kisiwani hapo walianza kushangilia ushindi huo. Hata hivyo, wakati wakiendelea kushangilia ushindi huo huku wakilidhihaki kundi lingine hali iliyosababisha warushiane mawe na mwishowe kuchomeana nyumba hizo.

Akizungumza na Nipashe, mmoja wa wananchi wa kisiwa hicho, Juma Ali, alisema kuwa wafuasi wa CCM waliokuwa wakisherehekea ushindi walikuwa wakiwazomea wafuasi wa wanaoaminika kuwa ni wa chama kingine na kuanza kupigana.


Alisema ugomvi huo ulizusha taharuki hadi kufikia wafuasi hao wa pande mbili kuanza kurushiana mawe hadi kuchomeana moto nyumba zao za makaazi yao.

“Kwa kweli hali ilikuwa mbaya katika kisiwa hiki cha Tumbatu hasa kijiji cha Tumbatu Gomani ambacho kina wafuasi wengi wa CCM na kijiji cha Tumbatu Chwaka ambacho kina wafuasi wengi wa chama kingine,” alisema. Alifafanua kuwa nyumba zilizochomwa moto ni za Gomani na Chwaka.

Kamishana wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame, alisema jumla ya nyumba tisa katika kisiwa hicho zimechomwa moto na chanzo cha ugomvi huo ni matokeo ya mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM.

Alisema tayari polisi kwa kushirikiana na vikosi vya SMZ, vimeshatuliza ghasia hizo kisiwani humo na pia wanaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini waliohusika na vitendo hivyo vya uvunjifu wa amani.

CHANZO: NIPASHE
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top