Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

SIMBA MABADILIKO KUIANGUSHA PRISONS

 Simba ilikuwa imegeuka kibonde wa Kagera Sugar pamoja na timu za Tanga na Mbeya, lakini msimu huu imezigeuzia kibao.
Kocha mkuu wa Simba, Dylan Kerr.
 
 
Baada ya kuvunja mwiko wa kuwa kibonde wa Mbeya City katika misimu miwili iliyopita, benchi la ufundi la Simba limetamba litaendeleza kaulimbiu ya 'mabadiliko' inayotamba nchini kwa sasa kwa kuibuka na ushindi dhidi ya Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya keshokutwa.
 
 
Simba ililazimishwa sare na Mbeya City katika mechi zote mbili za msimu wa kwanza (2013/14) wa timu hiyo ya Mbeya kushiriki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), kabla ya kuchezea kichapo katika mechi zote mbili za msimu uliopita wa ligi hiyo, 2-1 nyumbani na 2-0 ugenini, lakini juzi Wanamsimbazi walianza na kikosi chenye viungo watano, Said Ndemla, Jonas Mkude, Abdi Banda, Mwinyi Kazimoto na  Justice Majabvi na kuchomoza na ushindi wa 1-0 dhidi ya timu hiyo mjini hapa.
 
 
Ushindi huo ni mwendelezo wa mabingwa hao mara 18 wa Bara kufanya mabadiliko baada ya mwanzoni mwa msimu kuvunja mwiko wa kugawa pointi kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kwa misimu mitatu, safari hii wakichukua pointi sita kutoka kwa African Sports na Mgambo Shooting.
 
 
Mara tu baada ya kumalizika kwa mechi yao ya juzi jijini hapa, kocha msaidizi wa Simba, Seleman Matola, aliiambia Nipashe kuwa Tanzania Prisons ambao ambayo juzi ilisambaratishwa kwa kipigo kikubwa cha mabao 3-0 dhidi ya Stand United mjini Shinyanga, ijiandae kukumbwa na mabadiliko ya Msimbazi keshokutwa.
 
 
"Tumecheza vizuri kipindi cha kwanza, kipindi cha pili hali ya hewa ilitusumbua, lakini muhimu ni pointi tatu kwa sababu uwanja huu (Sokoine) umekuwa mgumu kwetu kwa kipindi kirefu. Tuko hapa Mbeya kwa ajili ya kuvunja mwiko na kupata pointi sita. Tayari tumepata tatu kwa Mbeya City, tunazisubiri pointi tatu nyingine kutoka kwa Prisons Jumatano," alitamba Matola.
 
 
Kuhusu mchezaji wa zamani wa Simba, Haruna Moshi 'Boban' ambaye juzi alicheza kwa mara ya kwanza VPL akiwa na kikosi cha City, Matola alisema: Hakuna asiyejua Boban ni mchezaji mzuri, tatizo linalomsumbua kwa sasa ni kwamba amenenepa, lakini akifanya mazoezi, atawasaidia sana Mbeya City."
 
 
Katika hatua nyingine, kocha mkuu wa Simba, Dylan Kerr, amekiponda kikosi chake kwa kuonyesha kiwango duni kwenye mechi yao ya juzi dhidi ya City.
 
 
Katika mahojiano na Nipashe jijini hapa jana, Muingereza huyo alisema: "Sijafurahishwa na namna timu ilivyocheza dhidi ya Mbeya City. Tulizidiwa kwa kiasi kikubwa, goli na ushindi pekee ndicho kitu cha kufurahia hapa, hatukucheza hivi kwenye mazoezi. Mechi haikuwa na furaha kwangu kwa sababu tumecheza soka la Amerika."
 
 
Kocha wa Mbeya City, Abdul Mingange, aliliambia gazeti hili jijini hapa juzi kuwa ili timu yake ifanye vizuri VPL msimu huu, watalazimika kusaka washambuliaji wakali wakati wa usajili wa dirisha dogo mwezi ujao.
 
 
"Tumetengeneza nafasi nyingi za mabao, lakini safu yetu ya ushambuliaji imetuangusha. Tunatakiwa kulitumia vyema dirisha dogo kuongeza washambuliaji," alisema meja huyo mstaafu ambaye msimu uliopita alikinoa kikosi cha Ndanda FC ya Masasi, Mtwara.
 
 
CHANZO: NIPASHE
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top