Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TAIFA STARS WAIBAMIZA MALAWI


Mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza la Taifa katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Malawi jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Samatta alipiga goti kwenye mstari wa lango na kuonyesha namba ya bukta yake (10) kwe wenzake.  Katika mechi hiyo ya kwanza ya mchujo wa kufuzu Kombe la Dunia, bao lingine akifunga mvaa jezi namba 11, Thomas Ulimwengu ambaye kama Samatta wanachezea TP Mazembe ya DRC.

Tanzania na Kenya zimeanza kampeni ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi kwa ushindi.
Tanzania imeicharaza Malawi 2-0 katika mechi iliyochezewa uwanja wa kitaifa wa Benjamin Mukapa jijini Dar es Salaam.
Bao la kwanza la Taifa Stars limefungwa na Mbwana Samata dakika ya 18 na la pili na Thomas Ulimwengu dakika ya 22.
Nchini Mauritius, Kenya walikuwa na mteremko, wakiondoka na ushindi wa 5-2 dhidi ya wenyeji wao.
Harambee Stars ilitangulia kufunga kupitia Johanna Omolo dakika ya 18, Ajub Masika dakika ya 23 na Shakava dakika ya 49.
Mauritius hata hivyo walijikakamua na nusura wafanye mapinduzi baada ya kupata mabao mawili kupitia Sophie dakika ya 66 na Bru dakika ya 78.
Lakini Kenya walidhibiti tena mchezo kupitia bao la Michael Olunga dakika ya 87 na bao la pili la Omolo dakika ya 82.
Mechi kati ya Sudan Kusini na Mauritania, ambayo ilikuwa yao ya kwanza kabisa katika dimba la Kombe la Dunia, ilisimamishwa kutokana na mvua kubwa.
Wakati wa kusimamishwa kwa mechi hiyo mjini Juba, timu zote mbili zilikuwa sare 1-1, bao la Sudan Kusini likitoka kwa Dominic Abui Pretino na la Mauritania Boubacar Bagili.
Katika mechi nyingine, Burundi walilaza Ushelisheli kwa bao moja bila
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top