Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

WAZIRI MEMBE AWAHUSIA MABALOZI WA TANZANIA

Katika picha ya kwanza, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akiongea na Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali na Wakuu wa Idara/Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje. Wengine katika picha hiyo ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Liberata Mulamula. Waziri Membe aliwataka Mabalozi hao kuhakikisha kuwa mafanikio ya kidiplomasia ambayo Serikali ya awamu ya nne imeyapata yanadumishwa na kuendelezwa katika kiwango cha juu zaidi. picha nyingine ni Waheshimiwa Mabalozi waliohudhuria kikao hicho.


Mhe. Membe anaonekana akifurahia zawadi ya ramani inayoonesha mandhari mbalimbali za nchi ya Japan. Zawadi hiyo alikabidhiwa na Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Batilda S. Burian
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top