Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Kampuni ya vinywaji ya SBC Tanzania yashusha bei ya vinywaji vyao,sasa ni Ths. 500 tu!

o
DSC_2480
Mkurugenzi wa Mafunzo na Uelimishaji Kitaifa kutoka kampuni ya SBC Tanzania, Rashid Chenja akionesha  tangazo jipya linaloonyesha punguzo la bei ya soda zao kutoka Tsh. 600 hadi Tsh. 500 kwa waandishi wa habari (hawapo pichani)  bei ambayo inaanza kutumika sasa kuanzia leo. Wengine: Kushoto ni Roselyne Bruno Meneja Masoko wa kampuni hiyo na kulia ni Omary Mandaya Meneja mauzo wa kampuni hiyo. (Picha zote  na Andrew Chale, Modewjiblog).

Na Rabi Hume,Modewjiblog
Kampuni ya kutengeneza vinywaji ya SBC Tanzania imeshusha bei ya vivywaji vya Pepsi, Milinda, Mountain Dew na Mountain Dew kutoka shilingi 600 hadi 500 kwa ujazo wa milimita 350 na 300 na milimita 250 kuwa shilingi 400.
 
 
Akitangaza kushuka kwa bei hiyo,  mapema leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa mafunzo na uelimishaji kitaifa kutoka SBC, Rashid Chenja amesema sababu ya wao kushusha bei ya vinywaji vyao bei ni kuwapa nafasi wateja wao kutumia bidhaa hiyo kutokana na hali za kimaisha kuzidi kupanda.


Amesema kabla ya kufikia uamuzi huo walifanya utafiti kwa kuzunguka maeneo mbalimbali na kuchukua maoni ya watumiaji wa vinywaji vyao ambao wengi wao walipendekeza bei ya shilingi 500 kutokana na hali za kimaisha kuwa ngumu na pia 500 ni pesa ambayo haina usumbufu mkubwa hata katika upatikanaji wa chenji.

“Kabla hatujaja hapa kutangaza bei zetu mpya tulifanya utafiti kwenye sehemu mbalimbali kuhusu kinywaji chetu na wengi wametoa maoni wakitaka bei ishuke hali ya maisha ngumu na hata hivi 500 haisumbui kupata chenji hivyo tunatangaza rasmi kushusha bei ya vinywaji vyetu,” amesema Chenja.


Ameitaja mikoa ambayo inanufaika na punguzo hilo kuwa ni Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara na Zanzibar ambapo kwa sasa wauzaji wa bidhaa zao wameomba wamalize bidhaa walizokuwa nazo ndiyo waanze bei mpya na watakuwa wakinunua kreti moja kwa 9,400 na watakuwa wakipata faida ya 2,500.


Nae Meneja masoko wa SBC Tanzania, Roselyne Bomio amesema licha ya kushusha bei ya vinywaji hivyo pia wapo katika mchakato kuona jinsi wanavyoweza kushusha bei ya vinywaji vyao vya milimita 500 ambavyo kwa sasa vinauzwa shilingi 800 licha ya maeneo mengi kuwa wakiuza 1,000.
DSC_2460 
Mkurugenzi wa Mafunzo na Uelimishaji Kitaifa kutoka kampuni ya SBC Tanzania, Rashid Chenja akisisitiza jmbo juu ya bei za soda zao kutoka Tsh. 600 hadi Tsh. 500 kwa waandishi wa habari (hawapo pichani)  bei ambayo inaanza kutumika sasa kuanzia leo. Wengine: Kushoto ni Roselyne Bruno Meneja Masoko wa kampuni hiyo na kulia ni Omary Mandaya Meneja mauzo wa kampuni hiyo.
DSC_2457Wanahabari wakifuatilia tukio hilo..DSC_2458
DSC_2463
Wanahabari wakifuatilia tukio hilo la mapema le
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top