Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LIPUMBA AIBUKA SASA ATOKA KIVINGINE


prof+LipumbaAliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.
Na Gabriel Ng’osha
HATIMAYE mwenyekiti wa CUF aliyejiuzulu, Profesa Ibrahim Lipumba (pichani) ameibuka na kumgeukia rais wa awamu ya tano, Dk. John Pombe Magufuli ambaye anatarajiwa kuhutubia Bunge leo kwa kumuambia kuwa ana mzigo mzito kutokana na hali ngumu ya bajeti ya nchi.


Akizungumza jana na wanahabari katika ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni jijini Dar, Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli anakabiliwa na mambo kadhaa yakiwemo ya hali ngumu ya bajeti ya serikali kufuatia taarifa (iliyopo kwenye tovuti) ya Benki Kuu ya Tanzania kuonesha kuwa mwaka wa fedha 2014/2015 serikali ilipanga kukusanya mapato ya ndani ya shilingi bilioni 12,178, sehemu kubwa ikiwa ni makusanyo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na badala yake serikali ilikusanya shilingi bilioni 10,507.

dk magufuli 
Rais Dk. John Pombe Magufuli.
Alisema mapato halisi ni madogo ukilinganisha na bajeti kwa kiasi cha shilingi bilioni 1,671 sawa na asilimia 14 ya malengo ya bajeti ya serikali.


Aliongeza kuwa halmashauri za wilaya, miji na majiji zilitarajiwa kukusanywa shilingi bilioni 458.5 lakini zilifanikiwa kukusanywa shilingi bilioni 360.1 sawa na asilimia 78. ya malengo ya bajeti.


Kwa upande wa misaada, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalam wa uchumi alisema kuna bajeti ya shilingi bilioni 1,481 lakini zilitolewa shilingi bilioni 1,024, upungufu ukiwa ni shilingi bilioni 457 sawa na asilimia 31 ya bajeti huku mikopo yenye masharti nafuu ya shilingi bilioni 1,000 ikafanikiwa kwa kupatikana shilingi bilioni 859.


Akizungumzia Tume ya Uchaguzi ya Zanziba (Zec), Lipumba amemtaka Rais Magufuli kutumia uamiri jeshi wake mkuu kuzungumza na kuishauri Zec kumtangazab mshindi wa urais na siyo kurudia uchaguzi kama serikali ya CCM Zanzibar inavyotaka.


“Kila kitu kiko wazi, mawakala walipata nakala za kila jimbo kwa majimbo yote 54, binafsi namuomba Rais Magufuli aishauri Zec itangaze matokeo halisi,”alisema Lipumba.


Aliongeza kuwa kwa kasi ya Rais Magufuli naungana naye katika kauli mbiu yake ya “Hapa Kazi Tu”, lakini alimtaka azingatie kauli nyingine ya “HAPA HAKI TU’’ili kuinusuru nchi isiingie kwenye machafuko yasiyo na msingi.


“Nampongeza kwa ziara zake za kushtukiza, tumeona zinazaa matunda mfano mzuri ni Hospitali ya Muhimbili baada ya kufika pale mashine za CT Scan na MRI zilitengemaa lakini ziara hizo hazitakuwa na tija kama bajeti ya maendeleo haikidhi matatizo ya Watanzania kama vile afya bora, elimu, ajira, kupambana na rushwa, miundo mbinu na kilimo ili kuwe na chakula cha kutosha nchini.


Aidha, Lipumba amempongeza Waziri Mkuu Mteule, Majaliwa Kassim Majaliwa kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo na Bunge kumpitisha.


“Naweza kusema Majaliwa ni kama kaokota embe dodo chini ya mpapai, Rais Magufuli hajakosea sana kwani yeye ndiye kiongozi na mtendaji mkuu, hivyo aliyeteuliwa anafaa kufanya naye kazi kwa karibu zaidi. Ingawa inampasa ajenge uwezo mkubwa sana wa kuwaongoza na kuwakabili wabunge pamoja na baadhi ya vigogo ambao nao walikuwa wanategemea wachaguliwe uwaziri mkuu,” alisema.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top