AtAsHx0mz7O0Tc_h4QgsCehoPZ7046db0BrjpXfGltty
Rais wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli akihutubia Bunge muda huu kutoka Bungeni Dodoma.

Na Andrew Chale, Modewjiblog
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh  Dk. John Magufuli anaelezea kuwa mambo yote vipolo atayatatua na kuifaya Tanzania kufikia malengo yake.

Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na suala la Katiba mpya ambayo amekili kuachiwa kiporo hivyo ataifanyia kazi ilikuikamilisha.

Suala la Muungano anaahidi kulifanyia kazi na kulitatua.

Awali:

Baada ya Rais kuingia Bungeni hali ilikuwa ni ya kelele na kuzomeazomea kwa wabunge lakini upepo huo ulitulia..Wabunge wa Upinzani katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Watanzania Wanazomea Bungeni mara baada ya Kutangazwa Kuingia kwa Rais wa Zanzibar Mh Dk Ali Mohamed Shein.


Wanachopinga wabunge hao wanadai hawamtambui Dk Shein Kama RaisHalali wa Zanzibar.Hali hiyo ilianza pale Naibu spika alipomuita Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Kutengua Kanuni ili Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wameze Kuongozana  na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Magufuli wakati atakapokuja Kulihutubia Bunge na Kulizindua Rasmi ,Wabunge hao waliaanza Kupiga kelele Mara Baad ya Kutangazwa kuingia kwa Spika wa Baraza la Wakilishi Zanziba, Makamu wa Pili wa Rais ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  Pamoja na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar..