moi2
Pichani ni Mohammed Dewji  alipokuwa mgeni rasmi wa tamasha la Simba Day, akisalimiana na mmoja wa wadau kwenye jukwaa kuuna kulia ni Nyange Kaburu.  (Pichana Maktaba yetu).
 
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Lile dili la mfanyabiashara mkubwa nchini, Mohamed Dewji kununua hisa katika klabu ya Simba SC linaonekana kuiva baada ya makamu wa rais wa Simba kuzungumzia dili hilo kuwa ni jambo nzuri la linafaida katika soka la sasa.


Akizungumza katika kipindi cha E Sport kinachorushwa na E Fm, Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu alisema jambo hilo wanalizungumzia kuangalia uwezekano kama wanaweza kumruhusu bilionea Dewji kununua hisa katika klabu hiyo.


Kaburu alisema katika soka la sasa ni jambo nzuri kuruhusu wanachama wa klabu kununua hisa ili timu iweze kupata mapato mengi zaidi na kuwa na uwezo zaidi wa kujiendesha jambo linaloweza saidia timu kuwa imara kwa kuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote ambalo wanaona lina faida na timu.


“Kisoka la sasa inakuwa ni vizuri kuuza hisa kwa mashabiki wetu ili timu iingize mapato mengi na tuwe tunafanya biashara wakati tunazidi imarisha timu yetu na swala la Dewji tunalo muda mrefu sana amekuwa akitaka tumuuzie hisa tunalizungumzia,” alisema Kaburu.


Aliongeza kuwa baada ya uongozi na washauri wao wa jinsi ya kuingiza fedha (EAG) watawashirikisha na wanachama wa klabu na baada ya hapo watatoa tamko juu ya kuanza kuuza hisa.


Taarifa za Bilionea, Mohamed Dewji kutaka kuinunua klabu ya Simba zilianza kusambaa zaidi baada ya kuzungumzia azma yake ya kuinunua Simba katika kipindi cha Mkasi kinachorushwa na EATV na tangu hapo mashabiki mbalimbali wa klabu hiyo kuanza kutoa maoni huku mashabiki wengi wakionekana kuridhia Dewji kuinunua klabu yao wakiamini anaweza leta mabadiliko kwa kutangaza yupo tayari kutoa Bilioni 20 kuiboresha Simba.