Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LIVERPOLL WAMNYAPIA NYAPIA JACK WILSHERE IWAPO ATAKATAA MKATABA MPYA ARSENAL

ARSENAL wamempa ofa  kiungo huyo Muingereza lakini wameweka masharti mpaya ikiwemo kupunguza kiasi katika mshahara wake wa  pauni £90,000 kwa wiki.
Wilshere, mwenye Miaka 26, amekwama kwenye mazungumzo na Arsenal. lakini rekodi yake mbaya ya kuumia mara kwa mara inaonyesha mkataba wake mpya utategemea sana  na pafomansi yake uwanjani. 
Lakini  Jurgen Klopp yupo tayari  kumpa Wilshere mkataba wake wa sasa mwishoni mwa msimu akiwa mchezaji huru.
Klopp tayari ameshamchukua mchezaji mwingine wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain kwenye dili la pauni  £35 milioni.
Na inajulikana kwamba amekuwa akimuhusudu Wilshere ambaye anapambana kurudi kwenye timu ya Taifa ya Uingereza ili ashiriki World Cup.

Mjerumani huyo anamuhitaji kiungo huyo ili kuweza kuziba pengo  Emre Can ambaye anaonekana kuvutiwa na Juventus.
Can hajakubali kusaini kandarasi mpya Anfield  na Klopp amesema: “Wakati mwingine mchezaji anapenda kuona mkataba wake unafika mwisho, hili sio jambo zuri kwa Klabu ,lakini kipindi inabidi uikubali hali hiyo"


Gwiji wa Liverpool  Phil Thompson anaona  Wilshere  utakuwa ni usajili mzuri sana kwa wekundu hao.
Alisema: “Ningemchukua kuja Liverpool — ana uwezo mkubwa .”
“Nimekuwa nikimhusudu kwa muda mrefu.”
Maoni yake yaliungwa Mkono na mchezaji wa zamani wa Arsenal staa Paul Merson ambaye alisema: “Nadhani Liverpool watamchukua sio muda mrefu.”

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top