Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TAARIFA KUTOKA SIMBA:OKWI FITI KUCHEZA DHIDI YA STAND UNITED


 

Mshambuliaji wa klabu ya Simba, Emmanuel Okwi, anatarajiwa kucheza mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Stand United utakaopigwa tarehe 4 Machi,siku ya Ijumaa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Simba katika kurasa za mitandao ya kijamii jana Jumanne, Daktari wa timu, Yassin Gembe, pamaja na Afisa habari wa Simba Haji Manara amesema, Okwi anaendelea vizuri na huenda akacheza kwenye mechi yao ya Ijumaa dhidi ya Stand United endapo kocha ataamua kumtumia wamesema hali ya mchezaji huyo inaendelea vizuri na kuna asilimia kubwa ya kucheza Ijumaa.

''Okwi anaendelea vizuri sana tofauti na jana, kwa hali aliyonayo pamoja na tiba ambazo tumeshampatia ni asilimia kubwa sana kwa yeye kuwepo kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Stand United Ijumaa hii'' alisema Gembe.

Huku afisa habari naye akiandika kwenye kurasa yake kuwa “Okwi anaendelea vizuri aligongwa kidogo kwenye enka lakini anaendelea vizuri, kama mambo yatakuwa vizuri kesho atakuwa mazoezini. Wanachama wa Simba na mashabiki wasiwe na hofu, alipata jeraha dogo ambalo haliwezi kumsababishia akose mchezo unaokuja kama kocha ataamua kumtumia”-Haji Manara, afisa habari Simba.

Okwi aliumia katika mchezo uliopita dhidi ya Mbao FC katika ligi, na kupelekea kutolewa nje huku nafasi yake ikichukuliwa na Laudit Mavugo.

Mpaka sasa Okwi amefunga jumla ya mabao 16 katika michezo 19 ambazo Simba imecheza mpaka sasa katika msimu huu wa Ligi Kuu Bara.

“Timu inaingia kambini kesho kujiandaa kwa ajili ya mchezo dhidi ya Stand United Ijumaa Machi 2, 2018.”


author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top