Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

JOSE MOURINHO:TUSIPOSAJILI WACHEZAJI WENGINE WAWILI AU WATATU TUTAKUWA NA MSIMU MBOVU SANA

Manchester United itakabiliwa na 'wakati mgumu' iwapo haitaongeza mchezaji yeyote katika dirisha la usajili linalokaribia kufungwa Alhamisi Kocha Jose Mourinho.
Mashetani wekundu hao wamemaliza msimu wa maandalizi kwa kipigo cha goli 1-0 dhidi ya mabingwa wa Ujerumani  Bayern Munich jana Jumapili.
Javi Martinez alifunga kwa kichwa cha kuparaza kipindi cha pili na kuwapa ushindi huo Bayern mechi iliyotawaliwa na mabingwa hao.
"Bosi wangu anajua ninachohitaji na imebaki siku chache ,nitasubiri na kuona kama tutaongeza mchezaji ," Mourinho alikiambia kituo cha  MUTV.
"Vilabu vingine tunaoshindana nao wanatimu nzuri na imara sana. au wameimarisha kikosi vizuri sana kama Liverpool, ambao wamenunua kila kitu na kila mchezaji.
"Tusipoimarisha timu yetu vizuri huu utakuwa msimu mbaya sana kwetu."
United wameshasajili wachezaji watatu mpaka sasa  - Kiungo MBrazil Fred kwa £47m, Mlinzi wa Kireno  Diogo Dalot na golikipa chaguo la tatu  Lee Grant.
Manchester United wanataraji kufungua pazia la EPL na  Leicester City Uwanja Old Trafford siku ya Ijumaa.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top