Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

 


PICHA:SIMBA ILIVYOJIFUA KUJIANDAA NA NUSU FAINALI DHIDI YA AZAM FC

Kikosi cha Simba kimehamia mji wa Unguja ambako mchezowa nusu fainali kombe la mapinduzi dhidi ya AzamFC utapigwa. Simba imepeleka wachezaji wake wote muhimu 
kuelekea mchezo wake na Azam utakaopigwa hapo kesho saa 2:15 usiku kwenye dimba la Amaan. Hizi ni baadhi ya picha za wachezaji wakiendelea na mazoezi makali kuelekea mchezo huo.

YANGA YASHUSHA BONGE LA KOCHA

Luc Eymael: Always on the move 07 July 2019: Leaves El Gaish FC
🇪🇬
26 September 2019: Luc Eymael signs a 2 year deal with Black Leopards. South Africa
🇿🇦
27 December 2019: Resigns at Black Leopards 09 January 2020: Confirmed as Young Africans coach
🇹🇿

O-LEVEL PHYSICS PRACTICAL GUIDE

MABINGWA WA ULAYA MARA SITA (6) LIVERPOOL WAPOKELEWA KWA SHANGWE




LIVERPOOL NI KUSUKA AMA KUNYOA


Kikosi cha Jurgen Klopp kinafanya vizuri lakini wiki hii kitaanza kupata wakati mgumu kwenye safari yao ya kuwani ubingwa tofauti na timu za Manchester United,Man City,Arsenal,Chelsea  na Tottenham Hottspur.

Baada ya michuano ya UEFA Nations League kuisha wiki hii zinaingia wiki tatu mfululizo kuelekea Oktoba kabla ya wiki ya mapumziko kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa.

Katika vinara wa EPL wanaowania ubingwa wenye ratiba ngumu ni Liverpool.Hebu tuangalia kila timu ratiba yake ilivyo .
LIVERPOOL
Ina kazi ngumu,hilo halina ubishi.Hiki ndio kipindi kinachosemwa ya kwamba ni kipimo kwa klabu hiyo kama kweli ina ubavu wa kuwani Ubingwa itakapoikabili  Tottenham Hotspur, Chelsea na Manchester City.
Ugumu umekuja pale ambapo imejikuta ina ratiba ngumu ya EPL lakini ikajikuta inaanza UEFA  na Paris Saint-Germain na kuifuata Napoli , wakati huo ikiikaribisha Chelsea katika Carabao Cup.
Lakini pia ikiwa na mechi nyumbani na Southampton, ambapo Liverpool ilishinda mara moja katika mechi nne walizokutana pale  Anfield pale timu hizo zilipokutana.
Hapo Jurgen Klopp kwa mara ya kwanza itabidi aanze kupumzisha baadhi ya wachezaji na kuanzisha wengine ili kikosi chake kiweze vuka salama katika kipindi hiki.
Hizi ndio mechi za Liverpool ambazo zinaweza kuipa picha nyingine kabisa msimu huu ambapo itaanza  Sep 15: Tottenham (A), Sep 18: PSG (H) (Champions League), Sep 22: Southampton (H), Sep 25/26: Chelsea (H) (Carabao Cup), Sep 29: Chelsea (A), Oct 3: Napoli (A) (CL),  na kumaliza Oct 7: Man City (H).

Manchester City

Wakiwa wameanza vizuri dhidi  Arsenal, inatazamiwa  City watakuwa wameshinda mechi saba dhidi ya saba watakopokuja kumenyana na Liverpool mwezi  Oktoba.
Hakuna ubishi, City ana ratiba nyepesi ya EPL, UEFA pamoja na Carabao Cup.
Mechi za City Sep 15: Fulham (H), Sep 19: Lyon (H) (CL), Sep 22: Cardiff (A), Sep 25: Oxford (A) (CC), Sep 29: Brighton (H), Oct 2: Hoffenheim (A) (CL), kabla ya kupepetana Oct 7: Liverpool (H).

Tottenham Hotspur

Tottenham wamepangiwa ratiba ngumu ya Champions League kuliko Liverpool, kwa kuangalia mechi zao mbili za mwanzo kwenye grupu lake.
Carabao Cup droo nayo imekuwa rahisi kwake dhidi ya  Lilywhites, ukichukulia mechi hiyo kupigwa pale  MK Dons.
Lakini mechi yao ya wikiendi hii dhidi ya  Liverpool, EPL itatoa nafasi kwa kocha Mauricio Pochettino kukibadilisha kikosi chake
Spur itaanza wikiendi tarehe Sep 15: Liverpool (H), Sep 18: Inter Milan (A) (CL), Sep 22: Brighton (A), Sep 26: Watford (H) (CC), Sep 29:Huddersfield (A), Oct 3: Barcelona (H) (CL), Oct 6: Cardiff (H).

Manchester United

Jose Mourinho alirekodiwa akianguka pale Wembley siku ya jumamosi imejidhihirisha vivyo hivyo kwa United ambayo imejikuta ikiangukia pua kwenye mechi za mwanzo wa msimu.
Vipigo viwili vimeifanya United ikifanya vibaya na kuzusha gumzo kubwa dhidi yake na wachezaji mahiri klabuni hapo.Hivyo kipindi hiki ndicho muafaka kuinua morali ndani na nje ya klabu hiyo.
Siku ya jumamosi inafunga safari kuifuata  Watford kibarua inachotakiwa kukimaliza vizuri ili kuiona United ikipanda nafasi zaidi  katika EPL.
Tarehe  Sep 15: Watford (A), Sep 19: Young Boys (A) (CL), Sep 22: Wolves (H), Sep 25: Derby (H) (CC), Sep 29: West Ham (A), Oct 2: Valencia (H) (CL), Oct 6: Newcastle (H).

Chelsea

Kama Liverpool, vijana wa London wameanza kwa ushindi wa  100% EPL msimu huu.
Na wana mechi mbili  dhidi ya Liverpool katika mechi zijazo ambazo ni moja ya EPL na Carabao Cup ambazo inabidi ifanye vizuri katika kampeni ya kuwa na msimu mzuri.
Swali moja linabakia ni namna gani wataweza kuhimili kucheza  alhamisi Europa Ligi na Jumapili EPL  na ni namna gani Kocha  Maurizio Sarri anayachukulia haya mashindano.
Wikiendi hii Sep 15: Cardiff (H), Sep 20: PAOK Salonika (A) (CL), Sep 23: West Ham (A), Sep 25/26: Liverpool (A) (CC), Sep 29: Liverpool (H), Oct 4: MOL Vidi (A) (EL), Oct 7: Southampton (A).

Arsenal

The Gunners  kama wanavyojulikana walianza na mechi ngumu dhidi ya City na Chelsea, lakini toka hapo wameanza kubadilika.

Mechi zao zote za EPL zitakuwa ni zile zilizo songana sana kipindi hiki.
Japokuwa, Arsenal wamepata nafuu kwenye droo ya  Europa League ukweli ukiwa watacheza London mara moja siku ya jumamosi dhdi ya  Tyneside.
Sep 15: Newcastle (A), Sep 20: Vorskla Poltava (H) (EL), Sep 23: Everton (H), Sep 26: Brentford (H) (CC), Sep 29: Watford (H), Oct 4: FC Qarabag (A) (EL), Oct 7: Fulham (A).

MCHEZAJI BORA WA FIFA:CRISTIANO RONALDO, LUKA MODRIC NA MO SALAH KUWANI TUZO

Cristiano Ronaldo, Luka Modric na Mohamed Salah ndio wachezaji watatu wa mwisho ambao watawania tuzo la mchezaji bora wa Fifa mwaka 2018.
Tuzo hizo zinafanyika huku mshambuliaji wa Barcelona raia wa Argentina Lionel Messi, mshindi mara tano wa tuzo la Ballon d'Or amekosa kuorodheshwa katika tatu bora.
Pia hakuna mchezaji yeyote aliyekuwa kwenye kikosi cha Ufaransa kilichoshinda Kombe la Dunia.
Huku winga mreno Ronaldo ambaye ni mshindi wa mwaka 2016 na 2017, alishinda kombe la tano la ligi ya mabingwa na Real Madrid mwezi Mei kabla ya kujiunga na Juventus kwa pauni milioni 99.2.
Kiungo wa kati wa Real Madrid Luka Modric alitajwa kuwa mchezaji bora kwenye Kombe la Dunia mwaka 2018 wakati Croatia ilifika fainali dhidi ya Ufaransa.
Mo Salah anakuwa mchezaji wa kwanza wa EPL kuorodheshwa kwenye tuzo hizo kwa mara ya kwanza toka mwaka 2008, pale Cristiano Ronaldo aliposhinda. Pia ni mchezaji wa kwanza toka bara la Afrika kufika hatua hiyo ya tatu bora toka Samuel Eto'o alipojumuishwa mwaka 2005.
Mmisri Mo Salah alifunga mabao 44 huku Liverpooll ikifika fainali ya ligi ya mabingwa na kushindwa na Real Madrid.
Modric aliwashinda Ronaldo na Salah kwa kushinda tuzo la mwanamume bora wa mwaka wa Uefa wiki iliyopita.
Mshambuliaji wa England Harry Kane ambaye alishinda kiatu cha dhahabu kwenye Kombe la Dunia alikuwa kwenye orodha ya kumi bora lakini amekosa.
Didier Deschamps, ambaye aliiongoza Ufaransa, ameteuliwa kuwania tuzo la kocha wa mwaka, akiwemo raia wa Croatia Zlatko Dalic na meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane.
Tuzo hizo ni kando la Ballon d'Or, baada ya shirikisho la kandanda duniani kukata uhusiano wake na tuzo hilo mwaka 2016.
Jopo la wataalamu wa Fifa waliunda orodha ya wachezaji 10 kwa kila tuzo huku manahodha wa timu za taifa, waandishi wa habari na mashabiki wakimchagua mshindi kila kundi likiwa na asilimia 25 ya kura.
Ni wachezaji nane(8) wa EPL ambao wamewahi kushiriki tuzo za mchezaji bora wa FIFA katika historia ambao ni – Lineker, Shearer, Bergkamp, Beckham, Henry, Lampard, Ronaldo, Torres.
Wachezaji wawili 2 waafrika ambao ni – Weah and Eto'o. Weah akishinda tuzo hiyo mwaka 1995, na Ronaldo mwaka 2008.
Washindi watatangazwa tarehe 24 Septemba huko Royal Festivan mjini London

NYOTA WAWILI PSG KUIKOSA LIVERPOOL



Liverpool wataikabili  PSG mnamo  Septemba 18 katika mechi ya ufunguzi UEFA mechi za makundi.
Kiungo wa  PSG  Marco Verratti atakosa mechi ya kwanza nyumbani kwa Liverpool huku kipa mkongwe Gianluigi Buffon naye akiangukia adhabu hiyo.
PSG watakuwa imara, wakiwategemea washambuliaji watatu Kylian Mbappe, Neymar na Edinson Cavani.
Huku Liverpool wakiwa tegemea  Virgil van Dijk, Alisson na Joe Gomez kukabiliana na wimbi la washambuliaji hao.

ZIJUE TAREHE MUHIMU UEFA CHAMPIONS LEAGUE


Real Madrid v Roma na  Liverpool v Paris ni mojawapo ya mechi zitakazokuwa na msisimko katika mechi za mwanzo hatua ya makundi.


Klabu Bingwa wa Ulaya (UEFA Champions League) hatua ya makundi tayari imepangwa na tarehe za michuano hiyo kuwekwa hadharani.

Mechi za ufunguzi zitaanza 

Jumanne 18 September
Kundi  A: Club Brugge v Dortmund, Monaco v Atlético
Kundi  B: Barcelona v PSV Eindhoven, Inter v Tottenham (both 18.55CET)
Kundi  C: Liverpool v Paris, Crvena zvezda v Napoli
Kundi  D: Galatasaray v Lokomotiv Moskva, Schalke v Porto
Jumatano 19 September
Kundi  E: Ajax v AEK Athens (18.55CET), Benfica v Bayern München
Kundi  F: Shakhtar v Hoffenheim (18.55CET), Manchester City v Lyon
Kundi  G: Real Madrid v Roma, Viktoria Plzen v CSKA Moskva
Kundi  H: Young Boys v Manchester United, Valencia v Juventus

Mechi kali zinatazamiwa kuwa 

Jumatano  3 October: Tottenham v Barcelona
Jumanne  23 October: Manchester United v Juventus
Jumanne  6 November: Inter v Barcelona
Jumatano  28 November: Paris v Liverpool
Jumatano 12 December: Ajax v Bayern München

Kuelekea Fainali  Madrid

18/19 September: group stage, matchday one
2/3 October: group stage, matchday two
23/24 October: group stage, matchday three
6/7 November: group stage, matchday four
27/28 November: group stage, matchday five
11/12 December: group stage, matchday six

17 December: Hatua ya 16 bora droo

12/13/19/20 February: round of 16 first leg
5/6/12/13 March: round of 16 second leg


15 March: robo-final na nusu -final droo


9/10 April: Quarter-finals, first leg
16/17 April: Quarter-finals, second leg


30 April/1 May: Semi-finals, first leg
7/8 May: Semi-finals, second leg

1 June: Final – Estadio Metropolitano, Madrid

KLABU BINGWA YA UEFA HATUA YA MAKUNDI

Hapo jana mida ya jioni kulikuwa na sherehe ya droo ya  kupanga makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya ,hivi ndivyo makundi yalivyo sasa.

Kundi A
Atletico Madrid, Dortmund, Monaco, Club Brugge

Kundi B
Barcelona, Tottenham, PSV, Inter Milan

Kundi C
PSG, Napoli, LIVERPOOL, Red Star Belgrade

Kundi D
Lokomotiv Moscow, Porto, Schalke, Galatasararay

Kundi E
Bayern Munich, Benfica, Ajax, AEK Athens

Kundi F
Man City, Shakhtar, Lyon, Hoffenheim

Kundi G
Real Madrid, Roma, CSKA Moscow, Viktoria Plzen

Kundi H

Juventus, Man United, Valencia, Young Boys
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top