Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

VIFAA VYA UFUATILIAJI KWA KUTUMIA SIMU ZA MKONO VYAPUNGUZA WIZI WA MAGARI NCHINI KENYA

Na Bosire Boniface, Wajir

Benjamin Waitathu Gikonyo alinunua gari aina ya Toyota Voxy rangi ya fedha mwezi Agosti uliopita kutoka kampuni ya Resma Motors mjini Nakuru Mkoa wa Bonde la Ufa nchini Kenya.

Mwanamke wa Kenya akitabasamu katika gari kongwe kwenye maonesho ya magari mjini Nairobi. Tangu mwaka 2011, madereva wameweza kuzilinda gari zao kwa kutumia vifaa vya kuzifuatilia kwa kutumia simu za mkono. [Na Roberto Schmidt/AFP]

Ili kujilinda uwezekano wa kuibwa na wezi, Gikonyo alinunua kifaa cha mfumo wa usalama kinachowawezesha wamiliki wa magari kutumia simu za mkononi kuzisimamia na kuzifanya gari zisiweze kufanya kazi iwapo zitaibwa.

Alisema kuwa ulikuwa uamuzi mzuri wa kuwekeza katika kifaa cha kufuatulia kwa sababu hapo tarehe 6 Novemba alipeleka ripoti katika kituo kikuu cha polisi kuwa gari yake ilikuwa imeibwa. Kwa kutumia mfumo wa usalama katika simu yake ya mkononi, Gikonyo aliweza kuifuatilia gari yake hadi huko Msitu wa Ngong Patakatifu karibu na mpaka wa Nairobi.

"Polisi na kampuni ambayo iliweka kifaa walinifuata hadi sehemu husika na kuipata gari yangu, Gikonyo aliiambia Sabahi. "Chombo kilipelekwa katika kituo cha Polisi cha Ngong na wahusika wanafanya uchunguzi ili kuweza kuwakamata wahalifu."

Gikonyo alisema kuwa teknolojia hiyo ilimuokoa uchungu wa kupoteza gari lake ambalo alinunua kwa shilingi milioni 1.2 (dola 14,000).

Wizi wa magari wapungua kwa asilimia 70 tangu mwaka 2010

Naibu msemaji wa polisi Charles Owino alisema kuwa ufuatiliaji vyombo kwa kutumia simu ya mkononi umesaidia kupunguza takriban asilimia 70 nchini kote katika miaka miwili iliyopita na kufanya kuwa ni kizuwio na kupelekea kutiwa mbaroni kwa watu wengi.

Kabla ya kufika kwenye soko la ndani kwa vifaa vya usalama vinavyodhibitiwa na simu mwaka 2011, wastani wa magari 15 yalikuwa yanaibwa kila siku nchini Kenya, aliiambia Sabahi. Sasa wastani huo umepungua hadi magari matano.


Pia, uchunguzi zinazopelekea kutiwa mbaroni kwa wezi zimeongezeka kutoka asilimia 10 mwaka 2010 hadi asilimia 60 hadi sasa mwaka huu, Owino alisema.

"Mapinduzi ya simu za mkononi yamefanya kupambana na uhalifu kuwa rahisi zaidi sasa kwa sababu ya kuwepo kwa ushahidi wa kumtia mtu hatiani," alisema.

Ingawaje wizi wa magari umepungua, wizi wa pikipiki umeongezeka katika kipindi hicho hicho, Owino alisema, akiwataka watoa huduma kuingiza sokoni vifaa kama hivyo kwa ajili ya wamiliki wa pikipiki pia.

Mwishoni mwa mwaka 2010, wizi wa magari ulihusika na upotevu wa shilingi bilioni 2.4 (dola milioni 28), na kufanya kuwa uhalifu mkubwa zaidi unaohusiana na mali za watu nchini Kenya, kwa mujibu wa Stephen Wambugu, wakala wa Shirika la Bima la Milltec, watoaji huduma nchini kwa ajili ya Kampuni ya Africa Merchant Assurance ya Kenya.

"Kwa sababu ya hali hiyo, makampuni ya bima yalillazimika kuongeza malipo ya bima zao za gari, lakini katika miaka miwili iliyopita imepunguka," aliiambia Sabahi.

Vifaa vya ufuatiliaji vinapunguza mzigo wa kifedha kwa makampuni ya bima na vinawaokoa wakati wa wamiliki wa mali kutoka kazini na kuanza kushughulika na polisi na makampuni ya bima, alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Garissa Mohammed Maalim alisema kuwa kifaa hicho pia kinahudumu kama kizuwio kwa wahalifu. "Wanaweza kuogopa kukamatwa kwa sababu maficho yao yanafuatiliwa, jambo ambalo pekee limeweza kuchangia katika kupungua kwa wizi," alisema.

Hata hivyo, alisema kuwa teknolojia sio hakikisho; kumekuwepo na kesi ambapo gari zilizoibwa hazikupatikana licha ya kuwekwa kwa mifumo ya ufuatiliaji.

Vifaa vya usalama kwenye simu vyawapa madereva udhibiti
Kampuni ya Sunrise Tracking Limited ni moja kati ya makampuni matano yanayoweka vifaa hivi, vinavyogharimu baina ya shilingi 10,000 (dola 118) na shilingi 30,000 (dola 353) kutegemea na mtoa huduma hiyo.

Mfumo huo wa usalama ni pamoja na teknolojia ya kuonekana kitu kilipo duniani ambacho kinawasaidia watumiaji kugundua wapi vilipo vyombo vyao. "Teknolojia hii inawaruhusu wamiliki kupelekewa taarifa wakati matukio yasiyotarajiwa kama vile ajali au kuingiliwa nyumbani kunapotokea," mkurugenzi mtendaji wa Sunrise Tracking Kelvin Macharia aliiambia Sabahi.

"Ikiwa mwizi anavunja chombo, vifaa vya kuhisi vinatambua tukio hilo na hutuma tahadhari katika simu ya mwenye chombo. Mmiliki anaweza kuita vyombo vya kusimamia sheria, jambo linaloweza kupelekea kutiwa mbaroni, au wanaweza kukifanya chombo kisifanye kazi kwa kutuma ujumbe," alisema.

Teknolojia hii pia inawaruhusu wamiliki kuangalia hali ya betri ya gari yao na mfumo wa kiyoyozi wa gari, na hata kusikiza mazungumzo ya watu waliomo katika gari, alisema.

Macharia alisema kuwa zaidi ya wateja 300, wakiwemo watu binafsi na mashirika, wamenunua mfumo huo tangu kampuni yao ilipoanza kutoa huduma hiyo mwezi Januari 2011.

Kampuni ya Mbetsa Innovations Limited pia inatoa teknolojia kama hiyo. "Kwa vile teknolojia hii ni mpya kabisa katika soko, wateja wamekuwa wakiongezeka kwa kasi," alisema Morris Mbetsa, ambaye anaongoza kampuni hiyo.

Mbetsa aliiambia Sabahi kuwa kila chombo kinapewa nambari tofauti ili kuhamasisha na kuifanya gari isiweze kufanya kazi ikiwa imeibwa. Watoaji huduma na wanaofunga vifaa hawawezi kupata habari hii.

Ingawaje kumekuwepo na vifaa vingine vya kufuatilia katika soko, alisema teknolojia inayohusiana na simu za mkononi ndiyo pekee ambayo inamruhusu mmiliki wa gari kuwa dhamana mwenyewe.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top