Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

SIMBA YAISHUSHIA KIPIGO MBAO,OKWI AKIZIDI KUWIKA

Simba imezidi kujikita kileleni mwa VPL baada ya kuishushia kipigo cha mbwa mwizi timu ya Mbao Fc kwa mabao 5-0 katika Uwanja wa Taifa.Ubabe wa Simba michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuipa dozi nene.

Katika mchezo huo ambao Simba waliutawala kwa asilimia kubwa, walianza kutikisa nyavu zake katika dakika ya 37 kupitia Shiza Kichuya, na dakika chache baadaye Emmanuel Okwi alifunga bao la pili kwa njia ya penati, baada ya kuchezewa faulo ikiwa ni dakika ya 41.

Mpaka dakika 45 za awali zinamalizika, Simba walikuwa kifua mbele kwa mabao 2-0.Huku ikionekana dhahiri shahiri Mbao Fc haikuwa siku yao hiyo.Simba ingevuna mabao zaidi iwapo umakini ungezingatiwa zaidi.

Kipindi cha pili kilianza  Simba wakionesha uchu wa kufunga zaidi, ambapo 69, Emmanuel Okwi alifunga tena bao, na kufikisha mabao mawili kwenye mchezo huo.

Na katika dakika ya 82, Erasto Nyoni aliongeza bao la 3, na baadaye kuelekea mwishoni mwa mchezaji, Nicoulous Gyan akapigilia msumari wa mwisho, kwa kufunga bao la 5.

Mpaka dakika 90 zinamaliza, Simba SC 5-0 Mbao FC.


Katika mchezo huo mshambuliaji wa Simba Emanuel Okwi ameivunja rekodi ya Simon Msuva na Abdulrahman Musa baada ya kufikisha magoli 16 kwenye ligi kuu Tanzania bara ikiwa ni mzunguko wa 19 raundi ya pili msimu huu (2017/18).

Ikizingatiwa mfungaji wa msimu uliopita 2016/17 waliangoza kwa mabao 14.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top